Kwa mujibu wa mdogo wake na mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha ITV, Ufoo Saro aitwaye Goodluck aliyekuwepo wakati wa tukio la mauaji lililotokea asubuhi ya jana, ambapo mchumba wa Ufoo alimuua mama yake mtangazaji huyo, na pia yeye kujeruhiwa kabla ya mtu huyo aitwaye Anthery Mushi kujiua pia.

“Tulisikia sauti ya risasi sebuleni…na hapo mama akawa anatuita anasema njooni hapa nakufa, tulipotoka nje tukakuta na dada nae ndo yuko chini, akatuambia rudini ndani anataka kutuua wote hawa, ndo tukarudi ndani. Baada ya kurudi ndani ndo akaanza kupiga risasi milangoni na madirishani akawa anasema tokeni nje nataka niwauwe,” Goodluck alikiambia kituo cha radio cha Times FM.
“Na sisi tukakimbia tukapanda juu dalini baada ya.........