AJTC NEWS

Thursday, February 7, 2013

MAMA LISHE WAWAOMBA WATEJA WAO KUWA WASTAARABU PINDI WANAPO TUMIA HUDUMA ZAO



wafanya biashara wadogo wadogo wa chakula maarufu mama rishe wa eneo la kwa morombo wamewaomba wateja wao kuwa wastaarabu pindi wanapotumia huduma zao

Hayo yamemwa na baadhi ya wafanya biashara walipokuwa wakihojiwa kwa nyakati tofauti na mmoja wa waandishi wa habari wa ajtc

Bi Fatma Ally ambaye ni mmoja wa mama lishe hao amesema katika biashara hiyo wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali ikiwemo na wateja kula chakula bila kulipa na kutoridhika na kipimo wanachopimiwa na mama lishe hao

Ameendelea kusema kuwa wateja hao ambao wengi ni wafanya kazi kutoka makampuni mbalimbali wamekuwa wakimwaga vyakula chini wakati wa kula na kusababisha uchafu katika eneo hilo

Pamoja na hayo Bi Susan Mabula ambae pia ni mmoja wa mama lishe hao hakusita kuelezea hasara wanayo ipata katika biashara hiyo ikiwemo na wateja hao kukopa chakula na kuchelewa kurejesha fedha hivyo kusababisha mama lishe hao kushindwa kununua bidhaa kama mchele na unga

Naye mmoja wa wafanya kazi hao ambaye ni mfanya kazi wa kampuni ya B AND B GEMS inayojishughulisha na madini Bw Heluman Amos amesema kuwa sio wote ambao wana tabia hiyo ila wapo wnye tabia kama hizo

Sanjari na hayo Bi Susan Mabula amemalizia kwa kusema anawashauri wakina mama wenzake kuwa na umoja katika yao


UCHAFUZI WA MAZINGIRA

kutokuwepo kwa utaratibu mzuri wa ukusanyaji taka katika eneo la mji mpya kwa morombo jijini arusha unaweza kupelekea kuwepo kwa magonjwa ya mlipuko

Akizungumza na ajtc radio Bi Eunicee Julius ambaye ni mmoja kati ya waathirika wa tatizo hilo amsema kuwa uchsfu huo umekuwa ni kero kutokana  na utupaji taka ovyo na kusababisha kuwpo kwa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu,kuhara na kutapika

Aidha Bi Eunice ameendelea kusema uchafuzi wa mazingira ni hatari hasa kwa wakazi waishio katika eneo hilo kutokana naile hali ya kutupa taka ovyo bila kujali afya zao

Pamoja na hayo Bi Eunice ameongezea kwa kusema kuwepo kwa utaratibu mzuri wa utupaji taka ili kuweza kuepuka magonjwa yanayozuilika kwa wakazi wa eneo hilo

Hata hivyo mwenyekiti wa eneo hilo Bw Lucas John amesema tatizo hilo liko mbioni kutatuliwa hivyo amewaomba wananchi kuwa wavumilivu ili kuwekwe utaratibu mzuri wa utupaji taka hizo

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA WAWEKEZAJI ILI KUTATUA TATIZO LA AJIRA



Wafanya biashara wa madini mkoani Arusha  wameiomba serikali kuongeza wawekezaji il kutatua tatizo la ajira kwa vijana

Akizungumza na ajtc redio kwa niaba ya wafanyabiashara wenzake bi careen saitoti ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya B&BGems amesema  biashara ya madini inaweza kuinua vijana endapo itawezeshwa

Pamoja hayo ameendelea kusema endapo serikali itaanda soko bora nchini itaweza kuinua sekta hiyo ya madini ili kuzuia ubadhilifu wa madini       Tanzania akitolea mfano kenya kuweka nembo ya nchi yao kwenye madini  ya tanzanite ili kuonekana wao ndio wazalishaji wakukk wa madini hayo ikiwa tanzania ndio nchi ya pekee inayozalisha madini hayo

Hata hivyo ameishauri serikali  kuwa kuwepo  na dhamana  ya uwekezaji,kuanda soko bora  la ndani na nje ya nchi,vilevile wawekezaji walete vifaa vya kukatia madini nchini il vijana wapate ajira

Amemalizia kwa kuishauri serikali iangalie upya utoaji wa leseni na vibali vya uhimbaji wa madini kwa wageni ili waweze kufanya biashara za madini kwa manufaa ya watanzania.