AJTC NEWS

Thursday, December 5, 2013

HIVI NDIVYO WATANZANIA WANAVYOMUENZI NELSON MANDELA

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela

Rais Jakaya Kikwete wa nchi hiyo pia ameagiza kuwa katika kipindi hicho cha siku tatu bendera zote zitapepea nusu mlingoti.
Kufuatia kifo hicho Rais Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini na kupitia kwake kwa mkewe Bi Graca Machel, wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika ya Kusini kufuatia kifo cha Mzee Nelson Mandela kilichotokea tarehe 5 Desemba, 2013 baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Rais ameuelezea msiba huu kuwa ni......

Monday, October 14, 2013

Simulizi kutoka kwa mdogo wa Ufoo Saro " Aliyemuua mama wa Ufoo Saro Alipanga kuua Familia Nzima"

Kwa mujibu wa mdogo wake na mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha ITV, Ufoo Saro aitwaye Goodluck aliyekuwepo wakati wa tukio la mauaji lililotokea asubuhi ya jana, ambapo mchumba wa Ufoo alimuua mama yake mtangazaji huyo, na pia yeye kujeruhiwa kabla ya mtu huyo aitwaye Anthery Mushi kujiua pia.
0L7C0700
“Tulisikia sauti ya risasi sebuleni…na hapo mama akawa anatuita anasema njooni hapa nakufa, tulipotoka nje tukakuta na dada nae ndo yuko chini, akatuambia rudini ndani anataka kutuua wote hawa, ndo tukarudi ndani. Baada ya kurudi ndani ndo akaanza kupiga risasi milangoni na madirishani akawa anasema tokeni nje nataka niwauwe,” Goodluck alikiambia kituo cha radio cha Times FM.
“Na sisi tukakimbia tukapanda juu dalini baada ya.........

Sunday, October 13, 2013

TUKIO KATIKA PICHA:MASKINI UFOO SARO AFANYIWA UPASUAJI WA KUONDOLEWA RISASI MWILINI APELEKWA WODI 12 YA KIBASILA.

 Ufoo Saro baada ya kufanyiwa upasuaji huo.
 Muuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), akimpeleka wodini Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufo Saro,  baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuondolewa risasi kufuatia kushambuliwa kwa silaha ya moto nyumbani kwa mama yake  Kibamba jijini Dar es Salaam leo na

Tuesday, August 27, 2013

SERIKALI YARUHUSU TENA MIHADHARA YA DINI ILIYOKUWA IMEPIGWA MARUFUKU.

MIHADHARA ya dini iliyokuwa imepigwa marufuku na Serikali imeruhusiwa kuendelea kwa masharti ya kutojihusisha na mahubiri yanayolenga kupandikiza chuki miongoni mwa Wakristo na Waislamu. Serikali pia imewataka viongozi wote wa dini kuwakataa na kuwapiga marufuku watu wanaojiingiza katika nyumba za ibada huku wakiwa na malengo ya siasa.

Akizungumza katika kongamano la Umoja wa Wahadhiri wa dini za Kikristo na Kiislamu Dar es Salaam juzi, Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja alisema Serikali haiwezi kuingilia shughuli za dini kama zinaendeshwa kwa ustaarabu bila kuvunja sheria.

Chagonja ambaye alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Dk. Emanuel Nchimbi alisema..........

MADIWANI WALIOTIMULIWA BUKOBA WARUDSHWA


 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.

Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya..........

Monday, August 26, 2013

HERI YA NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI.

Mavazi yanayodhamiriwa kuwa ni sehemu yakudhihirisha stara ya mwanadamu yageuka kuwa kipande cha karatasi ndani ya daftari .

Hayo yamebainishwa