Wafanya biashara wa madini mkoani Arusha wameiomba serikali kuongeza wawekezaji il kutatua tatizo la ajira kwa vijana
Akizungumza na ajtc redio kwa niaba ya wafanyabiashara wenzake bi careen saitoti ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya B&BGems amesema biashara ya madini inaweza kuinua vijana endapo itawezeshwa
Pamoja hayo ameendelea kusema endapo serikali itaanda soko bora nchini itaweza kuinua sekta hiyo ya madini ili kuzuia ubadhilifu wa madini Tanzania akitolea mfano kenya kuweka nembo ya nchi yao kwenye madini ya tanzanite ili kuonekana wao ndio wazalishaji wakukk wa madini hayo ikiwa tanzania ndio nchi ya pekee inayozalisha madini hayo
Hata hivyo ameishauri serikali kuwa kuwepo na dhamana ya uwekezaji,kuanda soko bora la ndani na nje ya nchi,vilevile wawekezaji walete vifaa vya kukatia madini nchini il vijana wapate ajira
No comments:
Post a Comment