AJTC NEWS

Thursday, January 10, 2013

MAKALA YA UJASIRIAMALI

MAKALA YA UJASIRIAMALI

Katika ulimwengu wa sasa kila kitu ni kujifunza tu mwenyewe ili uweze kuyamudu maisha ya sasa na ya baadae tukizungumzia swala la maisha ni lazima tugusie ujasiriamali

Hata hivyo ujasiriamali unaweza kujitokeza katika taswira tofauti lakini kwa lengo moja tu ili kuleta maendeleo ndani ya jamii yetu. iwapo kila mmoja kwa nafasi yake atajitokeza na kuweza kujishughulisha katika maswala mbalimbali ya kujipatia kipato kwa ajili ya kumudu au kukidhi mahitaji yake kimaisha.

Lakini kikubwa zaidi kabla ya kuendelea mbele ni lazima tujiulize swali kuwa ujasiriamali ni nini? kwani swala hili la ujasiriamali huwatatiza wengi hasa wale ambao hawajapata elimu hususani ile inayo jihusisha na ujasiriamali ama kwa lugha ya kizungu huitwa (ITERPRINUERSHIP) ambapo hii imetokana na lugha ya wenzetu wafaransa.

Ujasiriamali ni ile hali ya kuwa na ujasiri wa kuanzisha biashara kwa ujasiri bila kuogopa kitu chochote ama mtu yeyote kuwa atakuonaje ama atakuchukuliaje kwa njia yeyote ama mtazamo wowote.

 Sifa ya ujasiriamali haichagui kuwa wewe unataka kuanzisha biashara gani yaweza ikawa ni biashara ya ufugaji,kilimo, ama biashara yeyote ile ila lengo liwe ni kukidhi mahitaji yako au kujipatia kipato ambacho kitakutoa kutoka kwenye kipato kidogo mpaka kikubwa (Fanya fedha zako  ziendelee kuwa za kwako)


Ukiwa kama mjasiriamali kabla ya kuanzisha biashara kuna mambo makuu ya kuzingatia ikiwa ni pamoja kuwa na wazo ndipo mtaji ufuate. wazo lenyewe linatakiwa lihusishe biashara unayotaka kuifanya au kuanzisha kwa wakati huo.ukishajua ni biashara gani unataka kuanzisha  ni lazima ufanye utafiti ili uweze kujua hiyo biashara inagharimu kiasi gani cha fedha

Mtaji ni kiwango cha fedha ambacho wewe mjasiriamali unakiandaa kwa ajili ya kuendeshea biashara yako nakumbuka kuwa mtaji huo unaweza kuwa mdogo au mkubwa hii inatokana na uwezo wa mtu mwenyewe aliopanga kwa ajili ya hiyo biashara

Siku zote mtaji ndiyo jicho la biashara yako kwani unapoanzisha biashara unatakiwa isiporomoke au kuisha kabisa kwa maana hiyo mtaji hauna budi kulindwa kwenye biashara yoyote kubwa ama ndogo kwa hali yoyote ile mtaji ni lazima ulindwe na mjasiriamali ili lengo lake au ndoto zake ziweze kutimia na kuwa mjasiriamali mkubwa kwa kupitia uboreshaji wa biashara yake

Na katika biashara kuna makundi mengi ya biashara,kwanza kuna biashara ya mtu mmoja mmoja na kuna biashara ya makundi yaani [PATNERSHIP BUSINESS] ambapo ile ya mtu mmoja mmoja kwa na nafasi yake huitwa [PRIVATE BUSINESS] pamoja na nyingine nyingi kama limited company business

Makundi yote haya ya biashara huitaji mtaji kwa ajili ya kuendeshea biashara husika na kugharimu kiasi cha fedha kutokana ukubwa wa biaashara husika si haya tu bali makundi haya hutofautiana njia za umiliki na uendeshaji wa biashara ila yotee yanalengo moja tu za kuingiza faida na si vinginevyo

 
  MAKALA HII ITAENDELEA...................

No comments:

Post a Comment