AJTC NEWS

Wednesday, January 9, 2013

Rais wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha AJTC amewaonya wanafunzi kutochelewa chuo pindi wanapofungua chuo

ARUSHA

Rais wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha AJTC amewaonya wanafunzi kutochelewa chuo pindi wanapofungua chuo 

Hayo yamesemwa jana na rais  wa chuo hicho bwana david patric pindi alipokuwa akitoa adhabu kwa baadhi ya wanafunzi katika chuo hicho

Kuwepo na sababu za msingi pindi mwanafunzi anapochelewa kufika chuoni amesema hayo bwana Patric

Hata hivyo katibu wa chuo hicho bwana Michael Mosses amefanya juhudi ya kuwatafuta wale wote waliochelewa kufika chuoni na kuhakikisha wamepata adhabu ili kukomesha kitendo hicho cha uchelewaji chuoni hapo

Pia mmoja wa wanafunzi anaehusika katika uchelewaji huo ambae hakutaka jina lake lifahamike amesema kuwa uchelewaji wa wanafunzi ni kutokana na kutopewa mahitaji muhimu na wazazi wao kwa wakati husika

Mwanafunzi huyo amemalizia kwa kusema kuwa pamoja na adhabu zinazotolewa kutafutwe njia mbadala ili wazazi waweze kutoa mahitaji yao kwa wakati husika.  

No comments:

Post a Comment